Thursday, April 2, 2015


Wakazi wa Geita Pasaka hii watapata kuwaona live' Wasanii wa Kikundi mahiri cha KAPOTIVE Star Singers- Bukoba
TAMASHA hilo la PASAKA litafanyika Jumapili tarehe 05/04/2015 sikukuu ya Pasaka yenyewe katika ukumbi wa GEDECO, kuanzia saa 9 mchana hadi 2 usiku.
Kiingilio kwa watu wazima ni kununua tu DVD mpya inayoitwa KAPOTIVE LIVE SHOW kwa Tshs.10,000 tu. DVD hii inacheza pande zote mbili (Two in One). Watoto Tshs. 3,000 tu.
Karibuni sana tusherekee Pasaka kwa shangwe tukiwa na kundi zima la KAPOTIVE Star Singers-Bukoba. Mratibu wa Tamasha hilo Bw. Andrew Kagya akizungumza na Mwandishi wetu amewataka Wakaazi wa Mji wa Geita kuingia kwa Wingi katika Ukumbi huo ili kuburudika kwa Nyimbo za Injili na hapo hapo Mashabiki watajipatia DVD Mpya ya Kikundi hicho chenye makazi yake Mkoani Kagera.
Baadhi ya Waimbaji wa Kikundi cha Kapotive Star Singers wakiimba na kucheza wimbo wa Kihaya ambao ni moja ya Nyimbo zilizopo kwenye DVD hiyo mpya.

0 maoni:

Post a Comment

waliotembelea blog