Thursday, April 2, 2015


Jumamosi Signal Iduna Park itakuwa na kivumbi kikubwa wakati Wenyeji Borussia Dortmund watakapocheza na Mahasimu wao wakubwa wa Miaka ya hivi karibuni Mabingwa Bayern Munich.
Licha ya kuwa Msimu huu Bayern wanaelekea kuutwaa Ubingwa kilaini wakiwa Pointi 10 mbele kileleni na Dortmund kujikwamua toka mkiani na sasa wako Nafasi ya 10, Mechi hii Siku zote haikosi ushindani.
Hivi karibuni ushindani huu umeongezeka kwa uhasama baada ya Bayern 'kuwapora' Dortmund Mastaa wao Robert Lewandowski na Mario Goetze.
Pengine hali hiyo, ikichanganywa na kukumbwa na Majeruhi kibao, ndio ilisababisha Dortmund kupwelepweta Msimu huu.
Hali hii sasa imewageukia Bayern ambao wana Majeruhi wa Mastaa wao wakubwa, Arjen Robben, ambae ndie Mfungaji wao bora, na David Alaba huku Franck Ribbery akiwa na hatihati kucheza kutokana na maumivu.
www.bukobasports.comBUNDESLIGA
RATIBA
Jumamosi Aprili 4

16:30 Bayer Levkn v Hamburger SV
16:30 Eintracht Frankfurt v Hannover 96
16:30 Sport-Club Freiburg v 1. FC Köln
16:30 SV Werder Bremen v 1. FSV Mainz 05
16:30 TSG 1899 Hoffenheim v Borussia Mönchengladbach
16:40 VfL Wolfsburg v VfB Stuttgart
19:30 Borussia Dortmund v Bayern Munich

Jumapili Aprili 5
16:30 FC Augsburg v Schake
18:30 Hertha BSC v SC Paderborn 07

0 maoni:

Post a Comment

waliotembelea blog