Saturday, July 19, 2014

Kikosi-cha-Serengeti-Boys-Under-20 
TIMU ya taifa ya vijana chini ya umri wa miaka 17, Serengeti Boys imelazimishwa suluhu pacha ya bila kufungana dhidi ya  Afrika Kusini, (Amajimbo) katika mchezo wa kwanza wa raundi ya pili kuwania tiketi ya kucheza Fainali za Afrika za vijana.
Mchezo huo ulipigwa katika dimba la kisasa la Azam Complex, Chamazi, , Mbande, nje kidogo ya jiji la Dar es Salaam.
Katika mchezo huo, dakika 20 za kwanza, Afrika kusini walitawala na kulisumbua lango la Serengeti Boys, lakini mchezo huo ukabadilika na vijana wa Tanzania kuanza kusakata soka la uhakika.
Katika kipindi hicho cha kwanza, Serengeti walipata nafasi mbili za wazi, lakini washambuliaji wake walishindwa kuzibadili kuwa magoli.

0 maoni:

Post a Comment

waliotembelea blog