Saturday, July 19, 2014


EVERTON wanakaribia kumrudisha tena Romelu Lukaku katika dimba lao la Goodison Park.
Mbelgiji huyo ni mshambuliaji chaguo la kwanza la kocha Roberto Martinez  majira haya ya kiangazi na anatarajia kukamilisha usajili wake ndani ya saa 48 zijazo.
Martinez, aliyekuwa anamfikiria demba Ba kama mbadala wa Lukaku, hakukubaliana na mshahara aliodai wa paundi elfu 80 kwa wiki, na sasa anataka kumshawishi mbelgiji mwenye miaka 21 kumwaga wino katika kikosi chake cha msimu ujao.
Loan star: Lukaku impressed during his spell at Goodison Park last year and Martinez wants him back+4
Nyota wa mkopo: Lukaku alifanya vizuri alipokuwa Goodison Park mwaka jana na sasa  Martinez anahitaji huduma yake tena.
Target: Roberto Martinez has make Lukaku his priority as he looks to build on last season's impressive showing
Rada: Roberto Martinez amemweka Lukaku kuwa chaguo la kwanza katika usajili wa majira haya ya kiangazi baada ya kuonesha kiwango kikubwa msimu uliopita.

Inafahamika kuwa maandalizi makubwa ya kumrudisha Everton yamekamilika baada ya kurejea kutoka Austria walipoweka kambi.
Lukaku alikuwa anatarajia kusaini Atletico Madrid, lakini kwa bahati mbaya ikawa tofauti kwasababu hakuwa chaguo la kwanza la kocha Diego Simeone.
Wolfsburg  pia walionesha nia kubwa ya kumsajili kama ilivyokuwa kwa Tottenham, lakini Lukaku alifurahia maisha  Goodison na anapenda kuendelea kuisaidia klabu hiyo mpaka kufuzu ligi ya mabingwa.
Misfit: The Belgian striker has failed to make an impression at his parent club since joining in 2011
Majanga: Mshambuliaji huyu wa Ubelgiji ameshindwa kuonesha kiwango cha kuivutia klabu yake mama (Chelsea) tangu alipojiunga mwaka 2011.
Lethal: The striker netted 15 times in the league for the Toffees last year, and was their top scorer.
Mkali: Mshambuliaji huyu aliifungia mabao 15 Everton msimu uliopita na alikuwa ndiye mfungaji bora wa klabu.
Martinez pia amefanya mazungumzo ya kumrudisha mchezaji aliyekuwa kwa mkopo, Monaco, Lacina Traore.
Pia yupo katika makubaliano ya kumsajili kiungo wa Bosnia ,Muhamed Besic, mwenye miaka 21, anayekipiga klabu ya  Ferencvaros.

0 maoni:

Post a Comment

waliotembelea blog