Tuesday, February 11, 2014


STAA wa Bayern Munich Franck Ribery hataweza kucheza Mechi ya UCL, UEFA CHAMPIONS LIGI, Uwanjani Emirates wakati Arsenal na Bayern zitakapocheza Mechi ya Kwanza ya Raundi ya Mtoano hapo Jumatano Februari 19.

Vigogo hao wa Germany, ambao ni Mabingwa wa Nchi hiyo na pia ndio Mabingwa Watetezi wa Ulaya, wamethibitisha kuwa Ribery atakuwa nje kwa Wiki mbili baada Alhamisi iliyopita kufanyiwa upasuaji ili kuziba mshipa wa damu uliopasuka sehemu ya makalio yake.
Ribery, mwenye Miaka 30, anatarajiwa kurudi tena Mazoezini Wiki ijayo na hivyo kuikosa Mechi hiyo ya kwanza lakini atakuwa fiti kwa Mechi ya Marudiano na Arsenal itakayochezwa huko Allianz Arena Jijini Munich hapo Machi 11.
UEFA CHAMPIONS LIGI
Raundi ya Mtoano ya Timu 16
RATIBA
Jumanne Februari 18
22:45 Manchester City v FC Barcelona
22:45 Bayer 04 Leverkusen v Paris Saint-Germain
Jumatano Februari 19
22:45 AC Milan v Atletico de Madrid
22:45 Arsenal FC v Bayern Munich
Jumanne Februari 25
20:00 Zenit St. Petersburg v BV Borussia Dortmund
22:45 Olympiacos CFP v Manchester United
Jumatano Februari 26
22:45 Schalke 04 v Real Madrid CF
22:45 Galatasaray Spor Kulübü v Chelsea FC
MARUDIANO
Jumanne Machi 11
22:45 Bayern Munich v Arsenal FC
22:45 Atletico de Madrid v AC Milan
Jumatano Machi 12
22:45 FC Barcelona v Manchester City
22:45 Paris Saint-Germain v Bayer 04 Leverkusen
Jumanne Machi 18
22:45 Chelsea FC v Galatasaray Spor Kulübü
22:45 Real Madrid CF v Schalke 04
Jumatano Machi 19
22:45 BV Borussia Dortmund v Zenit St. Petersburg
22:45 Manchester United v Olympiacos CFP

0 maoni:

Post a Comment

waliotembelea blog