Tuesday, February 11, 2014

Ndege ya usafiri ya jeshi imeanguka ikiwa imebeba zaidi ya watu 100.
Redio ya taifa inasema ndege hiyo imeanguka katika eneo la milima katika jimbo la Oum El Bouaghi kusini mashariki mwa mji mkuu , Algiers na ilikuwa imewabeba abiria 103 wakiwemo wafnyakazi wa ndege hiyo.
Kuna taarifa kwamba ndege hiyo ilikuwa imebeba familia za maafisa wa jeshi.
Ndege hiyo ya wanajeshi inaripotiwa kuanguka katika eneo lililo na milima mingi mashariki ya nchi hiyo. Kituo cha Redio ya nchi ya Algeria inasema kuwa kulikuwa na waabiri 103, wakiwemo watumishi wa ndege hiyo.
Hakuna ripoti rasmi za majeruhi, ila vituo vya habari vya nchi hiyo vinapeana matumaini kwa uchache mno juu ya manusura.
Ndege hiyo inasemekana ilikuwa ikibeba wanajeshi na watu wa familia zao waliokuwa wakisafiri kuelekea jiji la Constatine. Jeshi halijatoa taarifa yoyote mpaka sasa.

Algeria imeanza siku tatu za maombolezi ya kitaifa kufuatia kuuawa kwa watu sabini na saba kwenye ajali iliyohusiha ndege moja ya Kijeshi Kaskazini Mashariki mwa nchi hiyo.
Abiria mmoja alinusurika ajali hiyo iliyohusisha ndege aina ya Hercules C-130 iliyoanguka katika eneo la milima ya Oum al-Bouaghi, ikiwa njiani kuelekea mji wa Constantine.
Ripoti zinasema hali mbaya ya anga ilisababisha ajali hiyo ya ndege.
Rais wa nchi hiyo Abdelaziz Bouteflika amewasifu wanajeshi waliopoteza maisha yao na kuwataja kama wafia dini wa taifa hilo.
Wengi wa abiria sabini na nane waliokuwa ndani ya ndege hiyo ni maafisa wa kijeshi na familia zao.
Mabaki ya ndege ya jeshi la Algeria iliyoanguka
Mwanajeshi aliyenusurika, anaripotiwa kuendelea kupokea matibabu katika hospitali moja mjini Constantine kufuatia majeraha ya kichwa.
Wizara ya Ulinzi imesema kuwa imeunda tume maalum kuchunguza ajali hiyo na kuwa Ahmed Gaid Salah, ambaye ni mkuu wa majeshi nba naibu waziri wa Ulinzi atazuru eneo la ajali hiyo.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotumwa kwa vyombo vya habari, wizara ya ulinzi imesema kuwa hali mbaya ya anga iliyohusisha kimbunga na mvua kubwa ya barafu ilisababisha ajali hiyo.
Runinga ya taifa ilionyesha picha za ajali hiyo.
Awali maafisa wa Ulinzi na shirika hilo la habari liliripoti kuwa watu 103 walikuwa ndani ya ndege hiyo lakini idadi hiyo ilipunguzwa hadi watu sabini na nane.





0 maoni:

Post a Comment

waliotembelea blog