Thursday, June 11, 2015



kuu wa wilaya ya Mufindi Mboni Mhita katikati akiwa katika picha ya pamoja na mabingwa wa mashindano ya kombe la Muungano Mufindi timu ya Mucoba Fc ,wa kwanza kulia ni mratibu wa mashindano hayo aliyestaafu rasmi Daud Yassin na mdau mkubwa wa soka mkoa wa Iringa Feisal Asas
Na MatukiodaimaBlog
MASHINDANO ya kombe la Muungano Mufindi yamefikia tamati baada ya timu ya benki ya wananchi wilaya ya Mufindi (MUCOBA FC) kuibukwa mabingwa wa fainali ya mashindano hayo kwa kuigagadua (kuifunga) timu ya Academ kutoka Dodoma kwa jumla ya magoli 2-0
Huku mratibu wa mashindano hayo Daud Yassin akitangaza kustaafu rasmi nafasi yake hiyo baada ya kuitumikia kwa miaka 19 hivi sasa .
Mratibu huyo aliweza kuwaaga rasmi wapenzi wa mpira wa miguu katika wilaya ya Mufindi mkoani Iringa baada ya kumalizika kwa mchezo huo wa fainali uliochezwa kwenye uwanja wa wa shule ya msingi wambi mjini Mafinga.
Yassin aliwashukuru wadau wote wa soka waliomsaidia kwa namna moja au nyingine kwa miaka 19 aliyoratibu mashindano hayo.
Alisema pia anawashukuru viongozi mbalimbali, chama cha soka wilaya ya Mufindi, chama cha soka mkoa wa lringa, shirikisho la soka nchi TFF, na ZFA kwa kuonyesha ukaribu wao kwa kipindi chote cha mashindano hayo.

0 maoni:

Post a Comment

waliotembelea blog