Thursday, June 11, 2015


Ukurasa wa mbele wa gazeti la The Sun leo umekuja na stori kwamba Manchester United wanahitaji mshambuliaji wa maana ili kurudi kushindania ubingwa msimu ujao.
Kwa mujibu wa The Currant Bun, “Manchester United wanakaribia kumsajili mshambuliaji wa Atletico Madrid, Mario Mandzukic”.
Mandzukic ameibuka kuwa mchezaji anayewaniwa zaidi na Man United ili kutengeneza muunganiko na Wayne Rooney msimu wa 2015/2016 chini ya kocha Louis van Gaal.
United wanalazimika kutafuta straika baada ya Radamel Falcao kurudi katika timu yake ya Monaco, huku Van Gaal akiwa hana mpango wa muda mrefu na Javier Hernandez na Robin van Persie.
Mario Mandzukic ni jibu kwa Van Gaal?
Mcroatia huyo alianza kuonesha cheche akiwa Bayern Munich na msimu uliopita alicheza vizuri akiwa na Atletico Madrid, lakini wachambuzi wengi wa soka hawamuweki kwenye kundi la washambuliaji wa kiwango cha juu zaidi duniani.

0 maoni:

Post a Comment

waliotembelea blog