Sunday, August 3, 2014


Packed to the rafters: 109,00 spectators watched the match unfold at Michigan Stadium in Ann Arbor
Nyomi ya hatari: Mashabiki 109,00 waliitazama mechi kwenye uwanja wa Michigan mjini Ann Arbor.

Louis van Gaal amekiri kuwa alikuwa na hofu ya ukubwa wa Manchester United baada ya kuwafunga Real Madrid mbele ya mashabiki 109,000 jana usiku nchini Marekani.
Van Gaal alisema: 'Tumecheza mbele ya mashabiki 300,00  kwenye ziara hii na watakuwa wengi zaidi katika mechi ya fainali mjini Miami (dhidi ya Liverpool jumatatu).
'Inashangaza sana na athari ya mashindano haya imekuwa kubwa mno zaidi ya nilivyowahi kuona katika maandalizi ya msimu nikiwa Ujerumani au Uholanzi.'
Full: The Michigan Stadium was jam-packed for United's exciting win against the European champions
Umefurika: Uwanja wa Michigan ulifurika mashabiki walioshuhudia United ikiwatandika mabingwa wa Ulaya.
Having a good time: Two United fans cheer on their team during the Guinness International Champions Cup
Furaha imerudi: Mashabiki wawili wa United walikishangalia kwa furaha wakati wa mechi ya kombe la kimataifa la  Guinness .

Van Gaal anaweza kushinda kombe la kwanza akiwa na United, ikiwa ni wiki tatu tu tangu aanze kazi na alisema: 'Huwezi kusema upo tayari kwa kuangalia mechi za maandalizi, lakini kiukweli ni matokeo mazuri na yanakufanya ujiamini'.
'Nilibalilisha wachezaji wengi kipindi cha pili na licha ya hivyo tulifunga tena.'
Alipoambiwa Liverpool ndio wapinzani wake wanaofuata, aliongeza: 'Nadhani ni jambo zuri kwa mpira wa Uingereza kuwa na timu mbili katika mechi ya fainali'
'Mechi hii dhidi ya Real ilikuwa kama si ya kirafiki, nilihisi Madrid hawakutaka kupoteza na ndio maana walimuingiza Ronaldo mwishoni tofauti na walivyopanga'

0 maoni:

Post a Comment

waliotembelea blog