Sunday, August 3, 2014


In trouble: 21 West Ham and Newcastle fans were arrested for fighting in Dusseldorf (not pictured)
 Mashabiki 21 wa Westham na Newcastle wamekamatwa na polisi mjini Dusseldorf (picha ya juu haihusiani na tukio).
POLISI nchini Ujerumani wamewatia mbaroni mashabiki 21 wa klabu za Westham na Newcastle baada ya kuanzishaji fujo na kuzichapa 'kavukavu' huko Dusseldorf.
Mapigano hayo yalizuku baina ya mashabiki hao hasimu jana mchana na polisi 100 walipelekwa eneo la tukio kutuliza ghasia.
Timu hizo mbili zitachuana katika kombe la Schalke 04 mwishoni mwa wiki hii huko  Gelsenkirchen.
Msemaji wa polisi wa Polizeipräsidium Düsseldorf alisema: 
"Kulikuwa na mashabiki 300 wa Uingereza katikati ya mji".
"Mashabiki kutoka klabu zote walikutana na awali ya yote walikuwa na bia na walipokutana walianza kurushiana maneno na baadaye kuamua kupigana".
"Tulituma polisi 100 katikati ya mji ili kutuliza mambo na zoezi hilo lilifanikiwa haraka na kwa muda mfupi tuliwatia mbaroni mashabiki 21",
Abroad: Newcastle and West Ham are competing in the Schalke 04 Cup this weekend
Mwishoni mwa wiki hii klabu za Newcastle na West Ham zinachuana katika kombe la  Schalke 04 

0 maoni:

Post a Comment

waliotembelea blog