Sunday, August 3, 2014

Louis van Gaal amejipa nafasi ya kutwaa kombe la kwanza akiwa Manchester United ikiwa ni wiki tatu tu tangu aanze kazi.
Kushindi kombe la kimataifa la maandalizi ya msimu nchini Marekani sio sababu ya kusema Man United itakuwa kali na kufuta machungu ya miezi 12 ya David Moyes, lakini utakuwa mwanzo mzuri kwa Mholanzi huyo katika dimba la Old Trafford kama timu yake itashinda fainali siku ya jumatatu mjini Miami.
Man United jana usiku imefanikiwa kuifunga Real Madrid  mabao 3-1, huku Cristiano Ronaldo akianzia benchi dhidi ya timu yake ya zamani.
Bao la kwanza la Man United lilifungwa na Ashley Young katika dakika 20. Katika dakika ya 27, Real Madrid walisawazisha bao hilo kwa mkwaju wa penalti uliotiwa kambani na Gareth Bale.
Katika dakika ya 37 kipindi hicho cha kwanza, Young aliifungia United bao la kuongoza na katika dakika ya 80, Javier Hernandez 'Chicharito' akaifungia United bao la tatu.
United's hero: Ashley Young struck twice to help his side beat the reigning European champions Real Madrid
Shujaa wa United: Ashley Young alifunga mawili katika ushindi wa 3-1
Packed to the rafters: 109,00 spectators watched the match unfold at Michigan Stadium in Ann Arbor
Watazamaji 109,00 waliitazama mechi kwenye uwanja wa Michigan mjini Ann Arbor

MATCH FACTS

KIKOSI CHA MANCHESTER UNITED (3-4-1-2): De Gea 7; Keane 5.5, Jones 7, Evans 6 (Blackett 45mins 6); Valencia 5.5 (Lingard 61mins 6.5), Herrera 7 (Cleverley 45mins 6), Fletcher 7.5, Young 7 (Shaw 45mins 6.5); Mata 6.5 (Kagawa 61mins 6.5); Welbeck (Zaha 41mins 5.5), Rooney 6 (Hernandez 61mins 7).

Mfungaji wa magoli: Young 20, 37, Hernandez 80.

KIKOSI CHA REAL MADRID (4-1-4-1): Casillas 6; Arbeloa 6 (Ronaldo 73mins 6), Pepe 6, Ramos 6.5, Fernandez 7; Alonso 7(De Tomas 55mins 7.5); Carvajal 6.5, Illarramend 6, Modric 6, Bale 7; Isco 6.

Mfungaji: Bale (pen) 27.

Kadi ya njano: Arbeloa, Isco.

Mwamuzi: Hilario Grajeda 7.
Breaking the deadlock: Young opened the scoring for United with a crisp finish past Casillas
Alivunja ngome: Young alimtungua kwa umakini mkubwa kipa wa Real Madrid, Iker Casillas

0 maoni:

Post a Comment

waliotembelea blog