Tuesday, May 20, 2014

IMG_1150 
Na Baraka Mpenja wa fullshangwe, Dar es salaam
WAGONGA nyundo wa Mbeya, klabu ya Mbeya City fc bado ipo jijini Dar es salaam kujiandaa na safari ya kwenda Sudan kushiriki michuano mipya ya CECAFA Nile Basin inayotarajia kuanza mei 22 mpaka juni 4 mwaka huu.
Kocha msaidizi wa klabu hiyo, Maka Mwalwisyi ameuambia mtandao huu kuwa asubuhi hii wanaendelea na mazoezi katika uwanja wa Kumbukumbu ya Karume jijini Dar es salaam.
“Ninavyozungumza na wewe muda huu tupo hapa Karume. Tunaendelea vizuri na mazoezi yetu. Na mambo yakikaa sawa muda wowote tutaanza safari ya kwenda Sudan”. Alisema Mwalwisyi.

0 maoni:

Post a Comment

waliotembelea blog