Tuesday, May 20, 2014

Wanachama-Simba 

HEKAHEKA za uchaguzi wa klabu ya Simba zinaendelea kwa kasi na ifikapo juni 29 mwaka huu rais mpya, makamu wa rais na wajumbe wa kamati ya utendaji watapatikana tayari kwa safari nyingine ya miaka minne.
Mwenyekiti wa kamati ya uchaguzi, wakili Dkt. Damas Daniel Ndumbaro jana aliweka hadharani majina 41 ya wagombea wa nafasi mbalimbali baada ya zoezi la uhakiki wa fomu kukamilika mwishoni mwa wiki iliyopita.
Hakuna jina lolote lililoenguliwa kwa sasa, lakini Ndumbaro alisema hayo ni majina ya awali na walichokuwa wanaangalia ni kama wagombea wamejaza fomu  vizuri na kuweka viambatanisho vyote.
Kwa wagombea wote walioomba kugombea nafasi zote zilizotangazwa walijaza vizuri fomu zao kwa mujibu wa mwenyekiti wa kamati ya uchaguzi.
Wakati Ndumbaro anataja majina hapo jana, nilishangaa kusikia maelezo yake kuwa kuna wanachama wa Simba wanamtaka awaache wagombea wote mpaka siku ya uchaguzi na wao ndio wataamua nani anafaa.

0 maoni:

Post a Comment

waliotembelea blog