Wednesday, January 11, 2017



MASHINDANO ya Kombe la Mataifa ya Afrika, AFCON 2017, yataanza Jumamosi Januari 14 huko Gabon na kushirikisha Nchi 16 zilizogawanywa Makundi Manne ya Timu 4 kila moja.

AFCON, ambayo Fainali yake itakuwa Februari 5, itachezwa kwenye Viwanja Vinne vya Miji ya Libreville, Franceville, Oyem na Port Gentil.
Viwanja vitakavyotumika ni Stade de l’Amitié huko Libreville, Gabon, unaochukua Watu 38,000, ambako Kundi A ndio litacheza Mechi zake, na kingine cha Kundi B ni Port Gentil Stadium, Port Gentil, wenye kuchukua Washabiki 20,000, Kundi C lipo Stade de Franceville Mjini Franceville wenye uwezo wa Watu 20,000 wakati Kundi D litakuwa huko Oyem Stadium ulioko Assok Ngomo, Gabon, uwezo 20,000.

Mabingwa Watetezi wa Afrika ni Ivory Coast lakini safari hii watawakosa Wachezaji wao wakubwa, wale Ndugu Toure, yaani Yaya na Kolo, ambao wamestaafu, na Majeruhi Yao Gervinho.



MAKUNDI:
KUNDI A:
Gabon, Burkina Faso, Cameroon, Guinea-Bissau
KUNDI B: Algeria, Tunisia, Senegal, Zimbabwe
KUNDI C: Ivory Coast, DR Congo, Morocco, Togo
KUNDI D: Ghana, Mali, Egypt, Uganda

Ivory Coast walitwaa Ubingwa wa Afrika huko Equatorial Guinea Mwaka 2015.

Wenyeji Gabon wapo Kundi A pamoja na Burkina Faso, Cameroon na Guinea-Bissau iliyotinga Fainali kwa mara ya kwanza.
Jirani zetu Uganda wapo kundi D pamoja na Ghana, Mali na Egypt ambao wanarejea kwenye Fainali hizi kwa mara ya kwanza tangu watwae Ubingwa Mwaka 2010.

AFCON 2017RATIBA
Mechi za Makundi
Jumamosi Januari 14
Kundi A

1900 Gabon v Guinea-Bissau
2200 Burkina Faso v Cameroon

Jumapili Januari 15
Kundi B

1900 Algeria v Zimbabwe
2200 Tunisia v Senegal

Jumatatu Januari 16
Kundi C

1900 Ivory Coast v Togo
2200 Congo DR v Morocco

Jumanne Januari 17
Kundi D

1900 Ghana v Uganda
2200 Mali v Egypt

Jumatano Januari 18
Kundi A

1900 Gabon v Burkina Faso
2200 Cameroon v Guinea-Bissau

Alhamisi Januari 19
Kundi B

1900 Algeria v Tunisia
2200 Senegal v Zimbabwe

Ijumaa Januari 20
Kundi C

1900 Ivory Coast v Congo DR
2200 Morocco v Togo

Jumamosi Januari 21
Kundi D

1900 Ghana v Mali
2200 Egypt v Uganda

Jumapili Januari 22
Kundi A

2200 Cameroon v Gabon
2200 Guinea-Bissau v Burkina Faso

Jumatatu Januari 23
Kundi B

2200 Senegal v Algeria
2200 Zimbabwe v Tunisia

Jumanne Januari 24
Kundi C

2200 Morocco v­­ Ivory Coast
2200 Togo v Congo DR

Jumatano Januari 25
Kundi D

2200 Egypt v Ghana
2200 Uganda v Mali

Robo Fainali
Jumamosi Januari 28

1900 Mshindi Kundi A v Mshindi wa 2 Kundi B
2200 Mshindi Kundi B v Mshindi wa 2 Kundi A

Jumapili Januari 29

1900 Mshindi Kundi C v Mshindi wa 2 Kundi D
2200 Mshindi Kundi D v Mshindi wa 2 Kundi C

Nusu Fainali
Jumatano Februari 1

2200 Mshindi RF 1 v Mshindi RF 4

Alhamisi Februari 2

2200 Mshindi RF 2 v Mshindi RF 3

Mshindi wa 3
Jumamosi Februari 4

2200 Aliefungwa NF 1 v Aliefungwa NF 2

Fainali
Jumapili Februari 5

2200 Finalist 1 v Finalist 2

NCHI ZILIZOWAHI KUTWAA UBINGWA WA AFRIKA:
-Egypt-Mara 7
-Cameroon, Ghana-Mara 4
-Nigeria-Mara 3
-Congo DR-Mara 2
-Zambia, Algeria, Congo, Ethiopia, Ivory Coast, Morocco, South Africa, Sudan, Tunisia-Mara 1

0 maoni:

Post a Comment

waliotembelea blog