Wednesday, January 11, 2017


Nusu Fainali ya Pili ya Kombe la Mapinduzi ambayo ni Mashindano ya kuenzi Miaka 53 ya Mapinduzi Tukufu ya Visiwa vya Zanzibar na Pemba, iliyokuwa Bigi Mechi, Dabi ya Kariakoo iliyohamia Amaan Stadium Zanzibar. Ilichezwa Usiku na Simba na Yanga kutoka 0-0 katika Dakika 90 lakini Simba kuibuka kidedea kwa Mikwaju ya Penati 4-2 na kutinga Fainali watakayocheza na Azam FC.
Katika Nusu Fainali nyingine iliyochezwa mapema Taifa Jang’ombe ya Zanzibar ilifungwa 1-0 na Azam FC kwa Bao la Dakika ya 33 la Frank Domayo.

Kwenye Mechi ya Watani wa Jadi, Timu zote zilishambuliana kwa zamu ingawa Yanga walionekana kutawala zaidi bila matunda yeyote na Gemu kuamuliwa kwa Mikwaju ya Penati Tano Tano.

Katika Penati hizo, Simba walifunga kupitia Kepteni wao Jonas Mkude, Kipa Daniel Agyei, Muzamil Yasin na Bokungu wakati ile iliyopigwa na Mwanjali kuokolewa na Kipa wa Yanga Munishi.

Penati za Yanga zilifungwa na Simon Msuva na Thabani Kamusoko na zile za Kipa Munishi na Mwinyi Haji ziliokolewa na Kipa wa Simba Daniel Agyei.

Fainali ya Mapinduzi Cup itachezwa Ijumaa Januari 13.

VIKOSI VILIVYOANZA:
YANGA:
Deogratius Munishi ‘Dida’, Juma Abdul, Mwinyi Haji, Andrew Vincent ‘Dante’, Kelvin Yondan, Saidi Juma ‘Makapu’, Simoni Msuva, Thabani Kamusoko, Amissi Tambwe, Haruna Niyonzima, Deusi Kaseke

SIMBA:
Daniel Agyei, Janvier Bokungu, Mohamed Hussein 'Tshabalala', Abdi Banda, Method Mwanjali, Jonas Mkude, Shiza Kichuya, James Kotei, Juma Luizio, Muzamil Yassin, Mohamed
Ibrahim

Mohamed Ibrahim akimtoka beki wa Yanga wakati mchezo wa nusu fainali ya kombe la Mapinduzi leo Usiku katika uwanja wa Amani, Simba wakifanikiwa kuingia hatua ya fainali baada ya kushinda kwa penati 4-2

Mshambuliaji wa Simba Laudit Mavugo akijaribu kumtoka beki wa Yanga Haji Mwinyi kwenye mchezo wa nusu fainali ya kombe la Mapinduzi leo Usiku katika uwanja wa Amani, Simba wakifanikiwa kuingia hatua ya fainali baada ya kushinda kwa penati 4-2­­
KOMBE LA MAPINDUZI
Ratiba/Matokeo:
Desemba 30, 2016

Taifa Jang'ombe 1 Jang'ombe Boys 0

Januari 1, 2017
KVZ 0 URA 2
Simba 2 Taifa Jang'ombe 1
 

Januari 2, 2017 Azam 1 Zimamoto 0
Yanga 6 Jamhuri 0

Januari 3, 2017
Jang'ombe Boys 2 URA 1
KVZ 0 Simba 1

Januari 4, 2017
Zimamoto 0 Yanga 2
Jamhuri 0 Azam 0

Januari 5, 2017
KVZ 1 Jang'ombe Boys 3
Simba 0 URA 0

Januari 6, 2017
Taifa Jang'ombe 3 KVZ 1

Januari 7, 2017

Jamhuri 0 Zimamoto 2
Yanga 0 Azam 4

Januari 8, 2017

Simba 2 Jang'ombe Boys 0
Taifa Jang'ombe 1 URA 0

Januari 10, 2017
Nusu Fainali

Azam FC 1 Taifa Jang’ombe 0
Simba 0 Yanga 0 [Penati 4-2]

Ijumaa, Januari 13, 2017
FAINALI

Saa 2: 15 Usiku
Azam FC v Simba

0 maoni:

Post a Comment

waliotembelea blog