Wednesday, January 11, 2017


EFL CUP
Nusu Fainali
Ratiba/Matokeo:
Jumanne Januari 10

Manchester United 2 Hull City 0

Jumatano Januari 11

22:45 Southampton V Liverpool
Manchester United, ikiongozwa na MenejaJose Mourinho, wamepiga hatua kubwa kuelekea kutwaa Taji kubwa la pili Msimu huu baada ya Jana huko kwao Old Trafford kuichapa Hull City 2-0 katika Mechi ya Kwanza ya Nusu Fainali ya EFL CUP, ambalo ndio Kombe la Ligi huko England.
Mwanzoni mwa Msimu, Man United walitwaa Ngao ya Jamii.
Juan MataBao za Man United, waliochezesha karibu Kikosi chao chote, zilifungwa na Juan Mata na Marouane Fellaini alieanzia Benchi. Markus HenriksenBao la Mata lilifungwa Dakika ya 56 alipounganisha Kichwa cha Henrikh Mkhitaryan na la pili Dakika ya 87 kupitia Fellaini alieunganisha Krosi ya Matteo Darmian. Wayne RooneyHull City na Man United zitarudiana huko KCOM Stadium hapo Januari 28. Jose MourinhoLeo Jumatano Januari 11 itachezwa Nusu Fainali ya Pili huko Saint Mary kwa Southampton kucheza na Liverpool.
Nusu Fainali hizi huchezwa kwa Mikondo Miwili ya Nyumbani na Ugenini na hivyo Marudiano ya Mechi hizi yatakuwa hapo Januari 25 na 26 huko Anfield na KCOM Stadium.

EFL CUP
Nusu Fainali
MARUDIANO
Jumatano Januari 25

23:00 Liverpool v Southampton

Alhamisi Januari 26
22:45 Hull City v Manchester United [0-2]

0 maoni:

Post a Comment

waliotembelea blog