Tuesday, October 13, 2015



Klabu ya Manchester United ya Uingereza ni moja kati ya vilabu vilivyotumia fedha nyingi katika dirisha la usajili lililofungwa mwezi August 2015. Toka kocha Louis van Gaal ajiunge na klabu ya  Man United, uongozi wa klabu hiyo umetumia zaidi ya pound milioni 250 kwa ajili ya kusajili wachezaji.
1D9FF5C700000578-0-image-a-43_1444732250406
Ed Woodward
Man United inaonekana kufanya usajili kwa malengo ya baadae zaidi kwani imekuwa ikisajili wachezaji wenye umri mdogo kama Memphis DepayAnthony Martial na Morgan Schneiderlin. Stori kutoka kwa makamu mwenyekiti wa klabu hiyo Ed Woodward kuhusu matumizi hayo ya fedha yaliyotumika katika usajili. 2CF1C2B400000578-0-image-a-44_1444732290529
Ed Woodward amekiri kuwa bado Manchester United itaendelea na matumizi ya fedha nyingi kwa ajili ya kuimarisha kikosi chake, Ed Woodward amesema Man United katika dirisha la usajili lililofungwa mwezi August walikuwa wakihusishwa kutaka kusajili wachezaji wengi zaidi lakini walifanikiwa kusajili sita. Hivyo Man United bado itaendelea kutumia fedha nyingi katika usajili ili kuimarisha kikosi.

0 maoni:

Post a Comment

waliotembelea blog