Saturday, September 12, 2015



Staa wa mchezo wa Tennis, Serena Williams na superstaa wa muziki wa Hip hop Drake wamekuwa topic kwenye mitandao mingi baada ya tetesi nyingi kusambaa kuwa wawili hao wapo kwenye mahusiano ya kimapenzi.
drake
Yote yalianza siku ambayo mapaparazzi walimnasa Drake kwenye picha akiwa kwenye mashindano ya Serena Williams huko Australia… haikuishia hapo, baada ya Serena kushinda Australia Open Championships, Drake alionekana tena kwenye mashindano yake ya French Open (Roland Garros), Wimbledon na haya ya jana U.S Open Championships.
drake2
Sasa jana staa huyo wa tennis aliweka headlines tofauti baada ya kukosa ushindi kwenye U.S Open dhidi ya Roberta Vinci wa Italy… Cha kushangaza zaidi mashabiki wamemshambulia Drake na kumlaumu sana kwa kitendo cha Serena Williams kukosa ushindi huo!
drake5
Mashabiki wanadai kuwa Drake amekuwa kikwazo kwenye mashindano haya na amemchanganya sana Serena kiasi cha kumfanya ashindwe kuweka akili yake yote kwenye mashindano hayo, mashindano ambayo kama Serena Williams angeshinda basi angeweka historia ya kuwa mwanamke mweusi kushinda mashinano yote hayo kwa mfululizo!
drake4
Nimefanikiwa kuzinasa baadhi ya tweets za mashabiki kwenye Twitter wengi wanatumia hashtag ya #BlameDrake kuelezea hisia zao..

0 maoni:

Post a Comment

waliotembelea blog