Saturday, September 12, 2015


Mabingwa Watetezi Barcelona na Real Madrid, Wikiendi hii wanarejea tena kwenye La Liga baada ya kusimama kwa Wiki 2 kupisha Mechi za Kimataifa na wote wapo Ugenini wakibadilishana Miji ambayo ndio makazi yao.
Jumamosi, Barcelona wako Ugenini huko Jiji la Madrid kucheza na Atletico Madrid Uwanjani Vicente Calderon wakati Real Madrid wako Jijini Barcelona kucheza na RCD Espanyol Uwanjani Estadi Cornellà-El Prat.
Mbali ya kubadilishana Miji, Barca na Real kila mmoja anamvaa Mpinzani wa Jadi wa mwenzake lakini kitu kingine cha kuvutia ni kutaka kuona kama Masupastaa wa La Liga, Cristiano Ronaldo na Lionel Messi kama wataweza kufungua hesabu zao za Magoli Msimu huu mpya baada ya kutoka kapa katika Mechi 2 za La Liga kwa Timu zao hadi sasa.
Kwa Wikiendi hii La Liga itaanza Ijumaa kwa Mechi 1 kati ya Levante na Sevilla na Jumamosi zipo Mechi 4 na Jumapili 4 huku Jumatatu ikichezwa Mechi 1.
LA LIGA
RATIBA
Ijumaa Septemba 11

2130 Levante v Sevilla FC
Jumamosi Septemba 12

1700 RCD Espanyol v Real Madrid CF
1915 Sporting Gijon v Valencia C.F
2130 Atletico de Madrid v FC Barcelona
2300 Real Betis v Real Sociedad
Jumapili Septemba 13
1300 Granada CF v Villarreal CF
1700 Athletic de Bilbao v Getafe CF
1915 Celta de Vigo v Las Palmas
2130 Malaga CF v SD Eibar
Jumatatu Septemba 14
2130 Rayo Vallecano v Deportivo La Coruna

0 maoni:

Post a Comment

waliotembelea blog