Thursday, September 17, 2015



Patashika ya michuano ya vijana chini ya miaka 12 ya Airtel Rising Stars ngazi ya taifa,
Patashika ya michuano ya vijana chini ya miaka 12 ya Airtel Rising Stars ngazi ya taifa baina ya Mwanza na Morogoro.

Patashika ya michuano ya vijana chini ya miaka 12 ya Airtel Rising Stars ngazi ya taifa, imeendelea kutimua vumbi katika dimba la Kumbukumbu ya Karume jijini Dar es Salaam, ambapo timu za Temeke na Mwanza zilipepetana kwa upande wa wasichana huku Mwanza na Morogoro walitifuana vikali kwa upande wa wavulana. 

Kwa kuanzia na mchezo ambao ulizikutanisha timu za wavulana, Mwanza waliwasambaratisha vibaya Morogoro kwa kuwashindilia magoli 3-1. Mwanza ambao walionekana kutakata kila idara, walijipatia bao la uongozi mnamo dakika ya 30 kupitia Lazaro Richard, baada ya kuitokea pasi nzuri iliyopigwa na David Richard na kumchambua vizuri kipa wa Morogoro kisha kuukwamisha mpira huo kimiani. 

0 maoni:

Post a Comment

waliotembelea blog