Tuesday, July 14, 2015



KOCHA mpya wa Real Madrid, Rafael Benitez ataonja joto ya pambano la watani Hispania, maarufu kama El Clasico wakati Los Blancos watapokutana na Barcelona kwa mara ya kwanza mechi ya mzunguko wa kwanza wa La Liga Novemba 8 Uwanja wa Bernabeu.
Mechi ya marudiano baina ya miamba hao walioweka kwenye 'viganja vyao' soka ya Hispania itafanyika April 3 mwakani, Uwanja wa Camp Nou.
Kocha Luis Enrique aloyeshinda mataji matatu na Blaugrana msimu uliopita, ataanzia kampeni yake ugenini kwa kumenyana na Athletic Bilbao Agosti 23 - mechi ya tatu ya wiki baina yao baada ya kikosi cha Ernesto Valverde kumenyana nao Barca mara mbili katika mechi za Super Cup. 
Lionel Messi alifunga katika mechi ambayo Barcelona iliifunga Atletico Madrid kujihakikishia taji la La Liga msimu uliopita

MECHI ZA UFUNGUZI LA LIGA

Athletic Bilbao vs Barcelona
Malaga vs Sevilla
Levante vs Celta Vigo
Sporting Gijon vs Real Madrid
Rayo Vallecano vs Valencia
Espanyol vs Getafe
Deportivo vs Real Sociedad
Granada vs Eibar
Real Betis vs Villarreal
Atletico Madrid vs Las Palmas 
Benitez yeye ataanza kampeni yake msimu huu kwa kumenyana na Sporting Gijon Uwanja wa El Molinon katika siku ya ufunguzi, wakati Malaga itaikaribisha Sevilla Uwanja wa La Rosaleda katika mechi ya mahasimu wa Andalucian.
Katika siku ya mwisho ya msimu wa 2015-2016, Mei 15, Real itasafiri hadi Galicia kuwafuata Deportivo La Coruna, wakati Barcelona pia watamalizia ugenini dhidi ya Granada, ambao walishika nafasi ya 17 katika msimu uliopita wa La Liga.
Kikosi cha Diego Simeone, Atletico Madrid chenyewe kitaanzia msimu mpya wa La Liga nyumbani wakiwakaaribisha Las Palmas na kumalizia nyumbani kwa Celta Vigo.
Atletico, ambayo msimu uliopita ilimaliza katika nafasi ya tatu ikiwa inazidiwa pointi na 16 na Barcelona, itamenyana na Real Madrid Uwanja wa Vicente Calderon Oktoba 4 na baadaye marudiano Uwanja wa Bernabeu, Februari 28

0 maoni:

Post a Comment

waliotembelea blog