Tuesday, July 14, 2015

Zuckernberg
Hakuna mtu hapendi kuwa na furaha mtu wangu, wapo wanaodhani kuwa ili uwe na furaha ni lazima uwe na pesa..  Mark Zuckerberg ni Mwanzilishi na Boss wa Facebook, yeye amesema kitu ambacho kinampa furaha mbali ya kuwa jamaa ni mtu na pesa zake nyingi tu.
“Kwangu furaha ni kufanya kitu kizuri na cha maana ambacho kinasaidia watu… Kuna watu wanachanganya furaha na kufurahia, naamini sio kitu rahisi kufurahia kila siku ila naamini inawezekana kufanya kitu cha muhimu ambacho kinasaidia watu kila siku” >>>  Mark Zuckerberg.
.
Mark Zuckerberg
Mark Zuckerberg amesema amefanikiwa kutokana na kuwa karibu na watu wake mara zote, kuanzia mkewe, washkaji zake wanaofanya wote kazi… anaamini pia hakuna mtu ambaye anaweza kuitengeneza njia ya mafanikio kwa kusimama pekeake, ila uhusiano mzuri na watu wanaomzunguka.
Kwenye tafiti inaonesha Mark Zuckerberg ana utajiri wa kama Bilioni 34.8… kama ulidhani furaha ni pesa basi haiko hivyo kwa  Zuckerberg.

0 maoni:

Post a Comment

waliotembelea blog