Friday, August 1, 2014


Diego Lopez ready to leave Real Madrid
DIEGO Lopez yupo tayari kuondoka Real Madrid majira haya ya kiangazi kwasababu ya kukosa namba ya kudumu katika kikosi cha kwanza.
Kipa huyo mwenye miaka 32 alijiimarisha chini ya Carlo Ancelotti aliyependelea kumuanzisha katika mechi za La Liga msimu uliopita, lakini alipoteza nafasi hiyo kwa kipa mwenzake Iker Casillas aliyekuwa anapangwa zaidi katika mechi za kumalizia msimu.
Kwa wiki kadhaa sasa, Madrid wanaiwinda saini ya kipa wa kimataifa wa Costa Rica, Keylor Navas na dili hilo litakamilika jumatatu baada ya rais wa Real Madrid, Florentino Perez kuwaomba Levante wacheleweshe uthibitisho mpaka kikosi kitakapokuwa kimerudi nchini Hispania kutoka katika kambi ya maandalizi ya msimu nchini Marekani.
Vyanzo vya habari vinasema, Lopez anaweza kuwa kipa namba tatu msimu ujao kwasababu watakuwepo makipa watatu wa kiwango cha juu.
Na ndio maana anataka kuondoka Santiago Bernabeu na anatarajia kuzungumza na Real Madrid baada ya kujua wapi pa kwenda.
Ancelotti ameshafikia maamuzi ya kumtumia kipa wa kimataifa wa Hispania, Iker Casillas kama chaguo la kwanza msimu ujao licha ya makosa aliyokuwa nayo msimu uliopita kwenye mechi ya nusu fainali ya ligi ya mabingwa na fainali za kombe la dunia nchini Brazil.

Muitaliano huyo hataki tena kubadilishabadilisha makipa kama alivyofanya msimu uliopita, hivyo nafasi ya Lopez inaonekana kuwa ndogo zaidi.

0 maoni:

Post a Comment

waliotembelea blog