Tuesday, December 10, 2013



MECHI ya Nusu Fainali ya Kombe la Mataifa ya
 Afrika Mashariki na Kati, CECAFA Challenge kati ya 
Tanzania Bara ‘Kilimanjaro Stars’ na Kenya ‘Harambee Stars’
 iliyopangwa kuanza Saa 7:00 mchana huu Uwanja wa Kenyatta, 
Machakos, imeahirishwa na sasa itachezwa Saa 12:00 jioni
 Uwanja wa Nyayo, Nairobi, Kenya.
1
Hii ndiyo hali halisi ya Uwanja wa Kenyatta, Machakos
6
Katibu wa Baraza la Vyama vya Soka Afrika Mashariki na
 Kati (CECAFA), Nicholas
 Musonye amesema kwamba sababu ya kufikia hatua hiyo 
ni hali mbaya ya Uwanja wa Kenyatta
 kufuatia mvua kubwa iliyonyesha leo.
Makocha wa timu zote, Kim Poulsen wa Tanzania Bara
 na Adel Amrouche wa Kenya wamekagua
 Uwanja na kujiridhisha haufai kuchezewa, ingawa 
Mwenyekiti wa Shirikisho la Soka Kenya (FKF) 
alikuwa anashinikiza mechi hiyo ichezwe hapo hapo.
Lakini pamoja na Musonye kutoa uamuzi huo, 
 Nyamweya amewaamuru wafanyakazi wa Uwanja
 wachote maji uwanjani aking’ang’aniza mechi ichezwe hapo.
2
Amrouche kushoto akimbishia Nyamweya mbele ya Musonye

3
Kim Poulsen ameweka msimamo hachezi Kenyatta
 
4
 
5




0 maoni:

Post a Comment

waliotembelea blog