Thursday, December 10, 2015



Baada ya mechi za hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Ulaya kumalizika usiku wa December 9 na kushuhudia vilabu 16 vikitinga hatua ya 16 bora na vilabu vingine 16 vikiaga mashindano hayo, December 10 ilikuwa ni zamu ya kushuhudia mechi za Europa League, miongoni mwa mechi za Europa League zilizochezwa usiku wa December 10 ni mchezo kati ya FC Sion ya Uswiss dhidi ya Liverpool ya Uingereza.
2831
FC Sion ndio walikuwa wenyeji wa Liverpool katika dimba lao la Stade de Tourbillon na kuwakaribisha Liverpool, licha ya kuwa FC Sion walikuwa katika uwanja wao wa nyumbani walionekana kutawaliwa na Liverpool kimchezo kwa  dakika zote 90, hata hivyo mchezo huo ulimalizika kwa sare 0-0.
3206
Hadi dakika 90 zinamalizika klabu ya Liverpool inayonolewa na kocha wa Kijerumani aliyewahi kuifundisha klabu ya Borussia Dortmund ya kwao Ujerumani Jurgen Klopp, walionekana kuutalawa mchezo kwa asilimia 61 na FC Sion ikimiliki mpira kwa asilimia 39 pekee. Liverpool licha ya kuutawala mchezo walishindwa kupata goli hata moja.
2754

0 maoni:

Post a Comment

waliotembelea blog