Wednesday, September 30, 2015


Baada ya Jana Klabu za Jiji la London, Arsenal na Chelsea, zote kubamizwa kwenye Mechi zao za pili za Makundi yao ya UEFA CHAMPIONS LIGI, UCL, Leo ni zamu ya Klabu mbili za Jiji la Manchester.
Leo, Manchester United wako kwao Old Trafford kucheza Mechi yao ya pili ya Kundi B na Klabu ya Germany VfL Wolfsburg.
Man United walifungwa Mechi yao ya kwanza huko Netherlands 2-1 na PSV Eindhoven.

Nao Man City, ambao wako Kundi D, walifungwa Mechi yao ya kwanza wakiwa kwao Etihad 2-1 na Juventus na Leo wako huko Germany kucheza na Borussia Monchengladbach.
Kwenye Mechi za Jana, Arsenal walipokea kipigo chao cha pili mfululizo kwenye Kundi lao baada ya kuchapwa Uwanjani kwao Emirates 3-2 na Olympiakos ya Greece.
Nao Chelsea, baada ya kushinda Mechi yao ya kwanza ya Kundi lao, Jana huko Ureno walipigwa 2-1 na FC Porto.

UEFA CHAMPIONS LEAGUE
RATIBA
Jumatano 30 Septemba 2015
KUNDI A

Malmö FF v Real Madrid
Shakhtar Donetsk v Paris St Germaine
KUNDI B
CSKA v PSV
Man United v VfL Wolfsburg
KUNDI C
19:00 FC Astana v Galatasaray
Atletico Madrid v Benfica
KUNDI D
Borussia Mönchengladbach v Man City
Juventus v Sevilla

0 maoni:

Post a Comment

waliotembelea blog