Wednesday, September 2, 2015



Klabu ya Manchester United imemsajili mshambuliaji mwenye umri wa miaka 19 kwa dau la pound milioni 36 akitokea klabu ya Monaco ya Ufaransa, Anthony Martial lakini mashabiki wamekuwa wakihoji kiwango hicho cha fedha kwa mchezaji huyo chipukizi, huenda ni kwa sababu hawa mfahamu.
2BE5EC8600000578-3219385-image-a-8_1441184638572
Martial ni mchezaji au mtu mwenye tabia za kupenda kukaa ndani, kupenda kupikiwa chakula na mama yake, ni mpenzi wa kuangalia Tv na kukaa na familia yake wakati ambapo anakuwa kamaliza kucheza mechi au kufanya mazoezi.
2BE5E9F700000578-3219385-image-a-14_1441184760864
Mshambuliaji huyo amemuoa Samantha na wana mtoto mmoja wa kike anaitwa Toto, huku wakitarajia kupata mtoto wa pili kwani mpenzi wake ni mjamzito kwa sasa. Dau la uhamisho wa Martial ambalo linafikia pound milioni 58 pamoja na bonus, linamfanya atajwe kama mchezaji mdogo mwenye thamani zaidi.
2BE5EF0C00000578-3219385-Martial_s_infant_daughter_Toto_dons_a_Monaco_kit_with_her_name_a-a-3_1441190703880
Martial ambaye watu na vyombo vingi vya habari za michezo hupenda kumlinganisha na mshambuliaji wa zamani wa kimataifa wa Ufaransa Thierry Henry, huwa na tabia ya kupenda kuchat na mpenzi wake muda mchache kabla ya mechi na kusikiliza muziki.
2BE5E15600000578-3219385-Martial_is_married_to_childhood_sweetheart_Samantha_and_the_coup-a-2_1441190703782
2BE676B500000578-3219385-image-a-2_1441188472682
2BE7396100000578-3219385-image-a-4_1441192866031
Hii ni video moja kati ya magoli yake aliyofunga akiwa na Monaco

0 maoni:

Post a Comment

waliotembelea blog