Tuesday, August 25, 2015

Klabu ya soka ya Simba mwishoni mwa wiki iliyopita ilimleta mshambuliaji wa kimataifa wa Senegal Papa Niang ambaye ni ndugu wa damu na Mamadou Niang mchezji aliyetamba katika vilabu kadhaa barani Ulaya ikiwemo timu ya taifa ya Senegal.
DSC_9335
August 24 Papa Niang alijaribiwa na wekundu hao wa msimbazi katika mechi ya kirafiki ya Simba dhidi ya Mwadui FC ya Shinyanga inayofundishwa na kocha Jamhuri Kiwelo, taarifa zilizotoka ni  kuwa Niang hajafanya vizuri majaribio ya Simba hivyo August 25 inaleta msenegal mwingine kuja kumfanyia majaribio.
Taarifa zinaeleza Simba inamleta Abdulah Ndow kutoka Senegal ila analetwa na wakala aliyemleta kocha wa Simba Dylan Kerr, msenegal huyo anayekuja Simba inadaiwa ameshawahi kucheza Ulaya katika klabu ya Bucharest ila alivunja mkataba baada ya kutolipwa fedha anazodai.

0 maoni:

Post a Comment

waliotembelea blog