Tuesday, August 25, 2015


Omar Wayne (aliyeruka juu) amepelekwa kwa mkopo Majimaji ya Songea
MAJIMAJI ya Songea mkoani Ruvuma imesajili wachezaji wawili wa Azam FC kwa mkopo wa muda mrefu wa msimu- beki Ismail Gambo ‘Kussi’ na kiungo Omary Wayne.
Wawili hao matunda ya akademi ya mabingwa hao wa Afrika Mashariki na kati tayari wamesafiri kwenda Songea kujiunga na Majimaji iliyorejea Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara msimu huu.
Wawili hao wanafanya idadi ya wachezaji watatu ndani ya wiki moja kutolewa kwa mkopo Azam FC, baada ya winga Joseph Kimwaga kupelekwa Simba SC jana.

0 maoni:

Post a Comment

waliotembelea blog