Tuesday, August 25, 2015

FULL TIME: ARSENAL 0 vs 0 LIVERPOOL, HAKUNA MBABE EMIRATES!

Kipa Petr Cech ndie aliyeilinda Arsenal usiku huu kutofungwa Alexis Sanchez akijituma
Wakati Liverpool hawajapoteza hata Mechi moja kwenye Ligi Msimu huu baada ya kushinda Mechi 2 na hii Sare na sasa wako Nafasi ya 3 wakifungana na Man United, Arsenal wao wako Nafasi ya 9 wakiwa wamefungwa Mechi 1, Ushindi 1 na Sare 1.
Arsenal walianza Ligi Msimu huu mpya kwa kufungwa Mechi yao ya kwanza 2-0 na West Ham wakiwa hapo Emirates na Wikiendi iliyopita kushinda 2-1 Ugenini walipocheza na Crystal Palace wakati Liverpool wameshinda Mechi zao mbili, kwa Bao 1-0 kila Mechi, walipocheza Ugenini na Stoke City na kisha Nyumbani Anfield na Bournemouth.
Cech akiokoa shuti langoni mwake lililopigwa na Benteke katika kipindi cha kwanza ambapo Arsenal na Liverpool zilibanana na kwenda mapumziko zikiwa 0-0.Ramsey akifanya yake, alifunga bao lakini mwamuzi alidai si bao kwani Ramsey alikuwa Ofsaidi

0 maoni:

Post a Comment

waliotembelea blog