Monday, April 13, 2015


LEO Jumanne Usiku Robo Fainali za UEFA CHAMPIONS LIGI zitaanza kwa Mechi mbili na moja ikiwa huko Jiji la Madrid, Spain ndani ya Estadio Vicente Calderon wakati Atletico Madrid watakapokuwa Wenyeji wa Mahasimu wao Real Madrid.Mechi hii, Dabi ya Madrid, maarufu kama El Derbi Madrileño, ni Marudio ya Fainali ya Msimu uliopita ya UEFA CHAMPIONS LIGI ambayo Real Madrid waliinyuka Atletico Madrid Bao 4-1 na kutwaa Ubingwa wa Ulaya kwa mara ya 10.

Mechi nyingine ya Jumanne Usiku itachezwa huko Jiji la Turin Nchini Italy wakati Wenyeji Juventus watakapoivaa AS Monaco ya France.

Real watatinga kwa maadui zao Vicente Calderon wakiwa na Kikosi kamili kwa mara ya kwanza katika Miezi Mitano.
James Rodriguez na Toni Kroos, ambao waliikosa Mechi ya La Liga ya Jumamosi walipoifunga Eibar 3-0 baada ya kuwa Kifungoni, wanarejea dimbani.

Nao Atletico wana habari njema ya kurejea dimbani baada ya kuzikosa Mechi mbili akijiuguza Enka kwa Straika wao Mario Mandzukic ambae tangu ahamie Atletico akitoka Bayern Munich mwanzoni mwa Msimu amepachika Bao 20 zikiwemo Bao 2 katika Gemu mbili dhidi ya Real Uwanjani Vicente Calderon.
Jumatano pia zipo mechi mbili nyingine za Robo Fainali ya UEFA CHAMPIONS LIGI kati ya PSG na Barcelona huko Mjini Paris na nyingine itachezwa huko Ureno kati ya FC Porto na Bayern Munich.

UEFA CHAMPIONS LEAGUE
Robo Fainali-Mechi za Kwanza
Jumanne Aprili 14

Atlético Madrid vs Real Madrid
Refa: Milorad Mažić (Serbia)

Uwanja: Estadio Vicente Calderón, Madrid, Spain
Juventus vs AS Monaco
Refa: Pavel Královec (Czech Republic)

Uwanja: Juventus Stadium, Turin, Italy

Jumatano Aprili 15
Paris Saint-Germain vs Barcelona

Uwanja: Parc des Princes, Paris, France
FC Porto vs Bayern Munich
Uwanja: Estádio do Dragão, Porto, Portugal


Fernando Torres akiwa na wenzake kwenye mazoezi huko  Vicente Calderon wakijiandaa na kipute cha UEFA leo Jumanne Usiku.

Fundi...! Meneja  Diego Simeone nae kwenye mazoezi

Simeone akiteta na Vijana wake wakati wa Mazoezi leo wakijiandaa vyema kuwakabili ndugu zao  Real Madrid leo Jumanne kwenye UEFA.

 Diego Godin, Arda Turan, Cristian Ansaldi, Antoine Griezmann na Torres wamejumuika leo kwenye zoezi

Simeone na Vijana wake hawajapoteza kwao Atletico Madrid kwenye mitanange sita tangu  2014 Champions League na leo wanaangalia kubaki na pointi
Wakiendelea na Mazoezi Vijana wa Klabu ya Atletico Madrid

Tiago na  Godin  nao kwenye mazoezi.

0 maoni:

Post a Comment

waliotembelea blog