Wednesday, March 18, 2015



Ligi Kuu Vodacom, VPL, Leo ipo dimbani kwa Mechi 3 za Jijini Dar es Salaam, Mbeya na huko Tanga huku Yanga wakiwa na nafasi poa kutwaa uongozi wakishinda.
Yanga Leo watakuwa Uwanja wa Taifa Jijini Dar es Salaam kucheza na Kagera Sugar na ushindi kwao utawashusha Mabingwa Watetezi Azam FC kutoka kileleni.


Lakini Kagera Sugar ni Timu ngumu ambayo katika Mechi ya kwanza ya Ligi Msimu huu iliichapa Yanga 1-0 huko Kaitaba, Bukoba.
Simba Leo hii wako huko Mkwakwani Tanga kuivaa Mgambo JKT wakiwa kwenye wimbi la ushindi wa Mechi 3 mfululizo kwa kuzichapa Tanzania Prisons 5-0, Yanga 1-0 na Mtibwa Sugar 1-0 ambalo limewafanya wajikite Nafasi ya 3.
Huko Sokoine, Mbeya, wana wa Nyumbani Mbeya City wataivaa Timu isiyotabirika Stand United ya Shinyanga.
VPL inaongozwa na Azam FC wenye Pointi 33 kwa Mechi 17 wakifuata Yanga wenye Pointi 31 kwa Mechi 16 na Simba ni wa 3 wakiwa na Pointi 29 kwa Mechi 18.

Kikosi cha Yanga
RATIBA YA MECHI ZA LEO:
Jumatano Machi 18

Yanga v Kagera Sugar
Mgambo JKT v Simba
Mbeya City v Stand United

0 maoni:

Post a Comment

waliotembelea blog