Tuesday, October 21, 2014


By Aidan Charlie Seif
FC Barcelona leo wanakutana na Ajax fc ya Uholanzi katika mechi ya ligi ya mabingwa wa ulaya – huku wakiwa wanataka kurudisha hali yao ya ushindi baada ya kupoteza mechi yao iliyopita dhidi ya Paris Saint-Germain.

637758
De Boer – Cocu na Enrique wakati walipokuwa wakiicheza FC Barcelona
Mechi hii inawakutanisha watu ambao falsafa za mchezo wa zinafanana – makocha wa timu hizi waliwahi kucheza pamoja katika kikosi cha FC Barcelona takribani miaka 15 iliyopita chini ya Louis Van Gaal.
Mechi za Nyuma
• Klabu hizi zilikutana kwa mara ya kwanza msimu uliopita, Barcelona walishinda 4-0 kwenye dimba la Camp Nou ambapo Lionel Messi alifunga hat trick – Ajax wakarudisha kisasi kwa kushinda 2-1 jijini  Amsterdam.
• Vikosi vilipangwa hivi msimu uliopita:
Barcelona: Valdés, Alves, Mascherano, Piqué (Bartra 80), Adriano, Busquets, Fàbregas (Xavi 71), Iniesta, Sánchez, Messi, Neymar (Pedro 72).
Ajax: Vermeer, Van Rhijn, Denswil, Moisander (Van der Hoorn 73), Blind (Schöne 78), Duarte, Poulsen, De Jong, Bojan, Sigthórsson, Boilesen.
TAKWIMU
Barcelona
• Kipigo cha Barcelona September 30 dhidi ya PSG ndio kilikuwa kipigo chao cha mapema zaidi katika Champions League tangu mwaka 2001.
• Barcelona wamepoteza mchezo mmoja tu wa nyumbani katika mechi 28 zilizopita za UEFA Champions League .
• The Blaugrana hawajahi kupoteza mechi ya nyumbani dhidi ya timu ya Uholanzi. Rekodi yao ipo hivi –  W4 D3 L0.
Ajax
• Baada ya kutoka droo ya 1-1 na APOEL, Ajax sasa wameshindwa kushinda mechi hata moja katika za ugenini Champions League – mara ya mwisho kushinda kwenye UCL ilikuwa ushindi wa  2-0 GNK Dinamo Zagreb October 2011.
• Frank de Boer alikuwa akicheza – na kaka yake Ronald alifunga – mara ya mwisho Ajax waliposhinda mechi ya UCL katika ardhi ya Spain baada ya kuifunga  3-2  Club Atlético de Madrid kaytika msimu wa 1996/97 UEFA Champions League hatua ya robo fainali.
• Ajax wamepoteza mechi zao 6 kati ya saba za mwisho walizocheza nchini Spain, wakitoa sare moja. Ushindi wao wa nyumbani dhidi ya FC Barcelona msimu uliopita ulikuwa ndio wa kwanza dhidi ya klabu ya Hispania tangu mwaka  2003/04.

0 maoni:

Post a Comment

waliotembelea blog