Tuesday, October 21, 2014


Kipindi cha Pili Man United walianza kwa kumtoa Ander Herrera na kumwingiza Marouane Fellaini ambae aliwapa manufaa makubwa kwa kusawazisha kwa Bao safi katika Dakika ya 48 na hilo ni Bao lake la kwanza kwa Man United katika Ligi.
Lakini udhaifu wa Difensi ya Man United, wakati wakiwa wanatawala Gemu, uliwapa WBA mwanya mkubwa kupiga Bao la Pili Dakika ya 66 kupitia Saido Berahino.
Man United waliweza kusawazisha Dakika ya 87 baada ya Krosi ya Rafael kuokolewa na kumkuta Daley Blind aliepiga kiakili kufunga. Sare hii imewaweka Man United Nafasi ya 6 wakiwa Pointi 10 nyuma ya Vinara Chelsea ambao Jumapili ijayo watatua Old Trafford kuivaa Man United katika mtanange unaongojewa kwa hamu.Fellaini akishangilia na Van Persie jana walipoingia na kutupia bao la kusawazisha..

0 maoni:

Post a Comment

waliotembelea blog