Friday, September 5, 2014


Rant: England boss Roy Hodgson has hit back at critics of his side following their win against Norway
Katukana: Bosi wa England, Roy Hodgson amejibu mapigo kutokana na kitendo cha kukosolewa baada ya kuonesha kiwango cha chini dhidi ya Norway

ROY Hodgson  amegeuka 'mbogo' baada ya kukosolewa kwa kitendo cha England kuonesha kiwango 'mbofumbofu' katika ushindi wa 1-0 dhidi ya Norway katika dimba la Wembley.
Kocha huyo aliulizwa kutoa maoni yake kutokana na timu yake kupiga mashuti mawili tu yaliyolenga lango katika mechi hiyo, na ndipo alipowaka mno akisema; "Sitaweza kuzungumzia hilo kwasababu kuna mtu ataniambia, "sawa, ulikuwa na mashuti mawili tu yaliyolenga lango" mie naona ni  f****** b*******, samahani." (hatujaona haja ya kutafsiri maneno hayo kwasababu za kimaadili).
Hodgson alionesha kisikitishwa na kiwango cha England katika uwanja wa Wembley na alikiri kuwa itawachukua miaka mingi kurudi katika kiwango cha zamani cha 'Simba watatu' wa ukweli.
Relief: Wayne Rooney's penalty earned England a slender win at Wembley
Mwokozi: Penalti aliyofunga Wayne Rooney iliwaokoa England wakiwa uwanja wa nyumbani wa Wembley
Spot on: Rooney's below-par display didn;t stop his burying the penalty kick
Kitu kambani: Rooney akimimina mpira nyavuni kwa mkwaju wa penalti.

Moyo wa Hodgson upo katika maandalizi ya mechi ya jumatatu ya kuwania kufuzu fainali za Euro 2016 dhidi ya Uswizi mjini Basle.
Hodgson amekuwa katika presha kubwa kutokana na mashabiki kukikosoa kikosi chake kwa kufanya vibaya katika fainali za kombe la dunia nchini Brazil ambapo waliambulia pointi moja tu katika michezo mitatu ya makundi.
Mashabiki 40,181 walihudhuria mechi ya jumatano-na hii ndio idadi ndogo zaidi kuwahi kutokea katika uwanja huo mpya tangu ulipozinduliwa mwaka 2007.

0 maoni:

Post a Comment

waliotembelea blog