Wednesday, August 6, 2014


Future doubt:  Arturo Vidal's move to Manchester United and Juventus could still go ahead
Hatima yake shakani: Bado dili la Man United kuendelea kumsajili Arturo Vidal linaendelea.



UHAMISHO wa Arturo Vidal kutoka klabu ya Juventus kwenda Manchester United umeingia shakani kwa sababu nyota huyo wa Chile hayupo fiti, hii ni kwa mujibu wa kocha wa timu ya taifa ya Chile.
Jorge Sampaoli, alikaririwa huko El Mercurio, akisema bosi wa Man United, Louis Van Gaal anaogopa kutumia paundi milioni 47 kumsajili kwasababu kiungo huyo ana matatizo ya goti.
Vidal kwa muda mrefu amekuwa akiwaniwa na Man United na ripoti zinasema kuwa dili hilo linakaribia kukamilika majira haya ya kiangazi.
Fitness worry: Chile boss Jorge Sampaoli says Louis van Gaal has doubts about the midfielder's knee injury
Hayupo fiti: Bosi wa Chile, Jorge Sampaoli anasema Louis van Gaal anaogopa kumsajili Vidal kwasababu ya majeruhi.

'Najua tatizo kubwa katika uhamisho wa Vidali wa dola za kimarekani milioni 80 (paundi milioni 47) kutoka Juventus kwenda Man United, ni Louis van Gaal kuwa na wasiwasi wa kuimarika kwa goti la Vidal,' Sampaoli aliliambia gazeti la Chile.
Vidal alifanyiwa upasuaji wa goti mwezi mei mwaka huu na aliharakishwa kupata matibabu ili kucheza fainali za kombe la dunia majira ya kiangazi mwaka huu nchini Brazil.

0 maoni:

Post a Comment

waliotembelea blog