Tuesday, July 29, 2014


Mourinho: It feels like Drogba never left Chelsea

JOSE Mourinho amefurahishwa na urejeo wa Didier Drogba na anatarajia mshambuliaji huyo ataisaidia Chelsea msimu uliopita. 
Mshambuliaji huyo wa kimataifa wa Ivory Coast alisaini mkataba wa mwaka mmoja ijumaa ya wiki iliopita kufuatia mkataba wake kumalizika na klabu ya Galatasaray ya Uturiki. 
Drogba alifurahia miaka nane akiwa darajani, kuanzia mwaka 2004 hadi 2012. 
Nyota huyo mwenye miaka 36 alijiunga na kikosi  cha Chelsea siku ya jumapi ambapo walishinda mabao 2-1 dhidi ya Olimpiji katika mechi ya maandalizi ya kabla ya msimu, lakini hakucheza.

“Awali ya yote, alipokuja, ilionekana kama hajawahi kuondoka klabuni,”  Mourinho aliwaambia waandishi wa habari. “Ilikuwa kawaida sana, hakukuwa na jipya kwasababu anamjua kila mtu na kila mtu anamjua”.

“Siku zote alikuwepo hapa hata kama hakuwepo hapa. Chelsea ni klabu yake,  hata miaka miwili ambayo alikuwa mbali na kuzichezea klabu za Galatasaray na Shanghai (Shenhua)”.


“Kwahiyo inaonekana kama alikwenda kwenye mapumziko mafupi na kurudi tena, kila kitu ni kawaida. Lakini kweli, nadhani tunamhitaji sana. Tunamtaka kaka mchezaji wa kikosi chetu ili kiwe kama ninavyotaka”.

0 maoni:

Post a Comment

waliotembelea blog