Sunday, March 16, 2014


 
Kikosi cha mabingwa wa soka Tanzania Bara, Yanga kimepata msukosuko baada ya basi lao kutumbukia msingini katika eneo la Mikese mkoani Morogoro.

Basi hilo limepata ajali takribani saa moja iliyopita wakati wakiwa njiani kurejea jijini Dar es Salaam baada ya mchezo wa Ligi Kuu Bara dhidi ya Mtibwa Sugar kwenye Uwanja wa Jamhuri mjini humo, jana.

Taarifa zinasema hakukua na majeruhi lakini baadhi ya wachezaji walilazimika kujiokoa baada ya basi hilo kulikwepa basi jingine ambalo lilikuwa linalifuata hilo la Yanga.
 

0 maoni:

Post a Comment

waliotembelea blog