Friday, February 14, 2014




FIFA Leo imetoa Listi ya Ubora Duniani na zile Nchi 3 za Juu, Spain, Germany na Argentina, bado ziko pale pale na Portugal kupanda nafasi moja na kukamata Nambari ya 4 huku Tanzania ikipanda Nafasi mbili na kushika Nafasi ya 116.
Brazil, Wenyeji wa Fainali za Kombe la Dunia hapo Juni, wamepanda Nafasi moja hadi Nafasi ya 9 lakini England imezidi kuporomoka na safari hii imeanguka Nafasi mbili na kuwa wa 15.
Nchi ya Afrika ambayo iko Juu kabisa ni Ivory Coast ambayo iko Nafasi ya 23 baada ya kuanguka Nafasi 6.

Listi nyingine ya Ubora itatolewa hapo Machi 13.
20 BORA:
1. Spain
2. Germany
3. Argentina
4. Portugal (+1)
5. Colombia (-1)
6. Switzerland (+2)
7. Uruguay (-1)
8. Italy (-1)
9. Brazil (+1)
10. Netherlands (-1)
11. Belgium
12. Greece
13. United States (+1)
14. Chile (+1)
15. England (-2)
16. Croatie
17. Bosnia-Herzegovina (+2)
18. Ukraine
18. France (+2)
20. Denmark (+5)

0 maoni:

Post a Comment

waliotembelea blog