Sunday, February 9, 2014

 

Ongeza kichwa

Jana naamini kwamba idadi kubwa wa washabiki wa ligi kuu ya Uingereza walishangaa kuona Arsenal walipata kipigo cha goli tano kwa bila dhidi ya Liverpool. Na Liverpool wamekuwa kileleni mwa dunia ya soka wikendi hii, lakini pia katika msimu huu nzima. Liverpool wamekuwa na msimu mzuri sana!
Hata hivyo, kutoka mwanzo wa msimu huu watu wengi wameamini Liverpool hawana uwezo wa kuchukua nafasi ya nne katika ligi. Liverpool hawajacheza Ligi ya Mabingwa tangu mwaka 2009! Lakini, msimu huu Liverpool wana timu ambayo naamini ina uwezo mkubwa wa kuchukua nafasi ya nne. Bila shaka Luis Suarez ni kati ya wachezaji bora katika Ligi Kuu ya Uingereza, na hata duniani! Lakini, washambuliaji wote Liverpool wameonyesha kiwango kikubwa kimpira msimu huu. Kwa mfano, Daniel Sturidge amefunga magoli 16 katika Ligi Kuu ya Uingereza!
Kitu ambacho naamini kinawasaidia Liverpool ni kwamba hawachezi katika Ligi ya Mabingwa . Kwa hiyo, tofauti na timu kama Chelsea, Manchester United, Arsenal, na Manchester City, Liverpool hawana sababu ya kupumzisha wachezaji katika Ligi ya Uingereza, na wachezaji wao hawachoki kutokana na kucheza mechi nyingi.

Mechi ya jana ilikuwa mechi ambayo niliamini kwamba Arsenal wangeonyesha kwamba kweli wana uwezo wa kushinda Ligi Kuu ya Uingereza. Ni mechi kubwa kama hii ambayo Arsenal wanahitaji kushinda kama kweli wanataka kuchukua taji la mabingwa wa Uingereza! Naamini jana Liverpool walicheza mpira mzuri sana na wa kushambulia. Lakini, sababu nyingine ambayo Arsenal ilifungwa ni ukweli wachezaji wachache walifanya makosa walipojaribu kuwakaba wachezaji wa Liverpool. Kwa mfano, Koscielny hakumkaba Skrtel vizuri wakati Liverpool walipopiga faulo katika dakika ya kwanza, na kwa hiyo, mchezaji huyu aliweza kuwafungia Liverpool goli la kwanza. Vile vile, Koscielny hakumkaba Skrtel kabisa katika corner ambayo Liverpool waliipata katika dakika ya kum, na Skrtel alifanikiwa kufunga goli lake la pili. Kocielny ni kati ya mabeki bora katika ligi kuu ya Uingereza, lakini, jana makosa yake yalisababisha Arsenal kupoteza pointi tatu.
Lakini , Arsenal bado wana nafasi nzuri ya kushinda ligi ya Uingereza. Kwa sasa wameshika nafasi ya pili nyuma ya Chelsea. Jumatano wanakutana na Manchester United. Arsene Wenger anajua, kwamba timu yake haiwezi kushinda ligi bila kushinda mechi kubwa!
Olle Bergdahl Mjengwa,
Stockholm.

0 maoni:

Post a Comment

waliotembelea blog