Friday, October 11, 2013

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. JAKAYA KIKWETE amewaagiza Wakuu wa Wilaya na Wakurugenzi wa Halmashauri zote nchini kuhahakisha kuwa shule zote za sekondari za kata, zahanati na vituo vyote vya afya nchini vinawekewa umeme haraka iwezekanavyo.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais, Ikulu imeeleza kuwa Rais KIKWETE amesema kwa maeneo yenye umeme wa Gridi ya Taifa, taasisi hizo za umma zipatiwe umeme kutoka kwenye Gridi hiyo na kwa maeneo yasiyokuwa na umeme wa Gridi basi shule na taasisi hizo nyingine ziwekewe umeme wa jua.

0 maoni:

Post a Comment

waliotembelea blog