Friday, October 11, 2013

Kampuni ya Ndege ya Fastjet imedaiwa kukiuka agizo la Mamlaka ya Usafiri wa Anga (TCAA) ya kutakiwa kukutana na mfanyabiashara Majaliwa Mbasa kumaliza mgogoro uliopo kufuatia kampuni hiyo kushindwa kumsafirisha kutoka Dar es Salaam kwenda Johannesburg, Afrika Kusini. Kwa mujibu wa barua ya TCCAA yenye

kumbukumbu namba TCAA/0.10/350/139 iliyoandikwa Oktoba 2 mwaka huu na kusainiwa na James Mabala kwenda kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Fastjet, mamlaka hiyo iliagiza kampuni hiyo kukutana na mfanyabiashara huyo ndani ya siku saba ili kuyapatia ufumbuzi malalamiko yake. Hata hivyo, Mbasa hadi kufikia juzi siku saba ilizotoa TCAA zikiwa zimeisha kampuni ya Fastjet ilikuwa haijamwita wala wakili wake kampuni ya Legal Clinics Advocate. Mmoja wa viongozi wandamizi wa kampinu ya Fastjet, Brown Francsi, alipoulizwa alisema halifahamu. Mbasa alisema alikata tiketi Septemba 23, mwaka huu kwa

0 maoni:

Post a Comment

waliotembelea blog