Monday, November 23, 2015


Jumanne Usiku Chelsea wako Ugenini kucheza Mechi ya Kundi G la UEFA CHAMPIONS, Dhidi ya Maccabi Tel Aviv wakiwa na matumaini ya kutinga Raundi ya Mtoano ya Timu wakiwa na Mechi 1 mkononi.
Hapo kesho, Chelsea wanaweza kufuzu wakiishinda Maccabi ambayo ishatupwa nje ikiwa Dynamo Kiev haishindi Mechi yao na FC Porto huko Ureno.
Na hata Sare kwa Chelsea inaweza kuwasaidia ikiwa FC Porto itaifunga Dynamo Kiev.
Chelsea wanatinga kwenye Mechi hii wakiwa kwenye morali nzuri baada ya Jumamosi kushinda Mechi yao ya kwanza ya kutoshinda Mechi 3 kwa kuifunga Norwich City 1-0 katika Ligi Kuu England.
Pia Chelsea wanarudiana na Maccabi ambayo waliitwanga 4-0 katika Mechi yao ya kwanza huko Stamford Bridge.
Lakini Maccabi, chini ya Kocha kutoka Serbia, Slavisa Jokanovic, ambae aliwahi kuichezea Chelsea na pia wanae Mchezaji wa zamani wa Chelsea, Tal Ben Haim, wameahidi kutia ngumu licha ya kuwa tayari wapo nje ya Mashindano haya.
UEFA CHAMPIONS LEAGUE
RATIBA 

Mechi  kuanza Saa 4 Dak 45 Usiku.
Jumanne Novemba 24

KUNDI E
20:00 BATE Borislov v Bayer Leverkusen
Barcelona v AS Roma
KUNDI F
Arsenal v Dinamo Zagreb
Bayern Munich v Olympiakos
KUNDI G
FC Porto v Dynamo Kiev
Maccabi Tel Aviv v Chelsea
KUNDI H
2000 Zenit Saint Petersburg v Valencia
Lyon v KAA Gent
Jumatano Novemba 25
KUNDI A
Malmö FF v Paris St Germaine
Shakhtar Donetsk v Real Madrid
KUNDI B
20:00 CSKA v VfL Wolfsburg
Man United v PSV Eindhoven
KUNDI C
18:00 FC Astana v Benfica
Atletico Madrid v Galatasaray
KUNDI D
Borussia Mönchengladbach v Sevilla
Juventus v Man City

0 maoni:

Post a Comment

waliotembelea blog