Thursday, October 1, 2015



Hii imekuwa kawaida kwa wanasoka wengi barani Ulaya kupenda kununua magari ya kifahari kutokana na mahitaji yao lakini hii huchangiwa na mishahara yao mikubwa wanayolipwa na vilabu vyao. Mapema mwaka 2015 tuliona nahodha wa klabu ya Chelsea John Terry alionesha gari lake jipya.
October 1 mshambuliaji wa kimataifa wa Brazil na klabu ya FC Barcelona ya Hispania Neymar ameonesha gari lake jipya aina ya  Ferrari 458 Spider, gari ambalo thamani yake inafikia pound 200000/= ambazo ni zaidi ya milioni 600 za kitanzania. Neymar kapiga picha na gari lake hilo la kifahari na kuweka katika account yake ya instagram.
2CF8F40300000578-3256270-image-a-32_1443706780157
Neymar akiwa na gari lake jipya Ferrari 458 Spider
Neymar ambaye ni moja kati ya wachezaji walioisaidia FC Barcelona kuibuka na ushindi wa goli 2-1 dhidi ya Bayer Leverkusen bila kuwa na staa tegemeo wa timu hiyo Lionel Messi, picha ya Neymar iliambatana na ujumbe huu >>>”asante mungu kwa kunipa afya na matunda ya kazi yangu kwa kutimiza ndoto yangu”

0 maoni:

Post a Comment

waliotembelea blog