Saturday, October 31, 2015

LIONEL MESSI WENDA AKAIKACHA SPAIN, KWENYE MIKAKATI YA KUJIFUNZA LUGHA YA KIINGEREZA! CRISTIANO RONALDO NAE YALE YALE...MAN UNITED, PSG KWENYE SAHANI MOJA ZIKIMHITAJI!

MCHAMBUZI wa kuheshimika wa Soka la Spain amedokeza kuwa Mastaa wakubwa Nchini humo, Cristiano Ronaldo na Lionel Messi, wako mbioni kutimka na ipo nafasi kubwa kwao kutua Ligi Kuu England.
Akiongea na Jarida la talkSPORT, Guillem Balague, Mwandishi na ambae pia ni Mchambuzi wa Sky Sports' kwenye Shoo yao Revista de la Liga, amesema upo mkakati kwa Ronaldo kuihama Real mwishoni mwa Msimu huu lakini si kurudi Manchester United bali kwenda Paris Saint-Germain.
Licha ya mwenyewe Ronaldo, mwenye Miaka 30, kutoboa hivi karibuni kuwa atastaafu akiwa na Real, Balague amekiri Ronaldo anaihusudu Man United lakini ipo dili ya yeye kuhamia PSG.
Balague ameeleza: “Ataondoka Real. Upo mkakati toka Watu wake kuondoka mwishoni mwa Msimu na PSG wanazo pesa na Real wako tayari kumwachia. Ronaldo anaihusudu Man United .. Mashabiki, hali ilivyo Old Trafford na Klabu, lakini sasa Klabu ipo kwingine. Je Man United watalipa Euro Milioni 125 pamoja na kumlipa yeye Milioni 20 kila Mwaka wakati huu? Kwanini watumie pesa hizo?”
Wakati huo huo, Guillem Balague pia ametoboa kuwa Lionel Messi sasa anajifunza Kiingereza kwa ajili ya uwezekano wa kuhamia Ligi Kuu England.
Messi, mwenye Miaka 28, amekuwa akihusishwa na kuhamia Chelsea, Manchester United na Manchester City hasa kwa vile hana raha huko Barcelona hasa baada ya kuandamwa na Kesi ya Ukwepaji Kodi Mahakamani Nchini Spain.
Balague ameeleza: “Bado hajaamua kuhamia, anafikiria kuhusu hilo. Ameshasikia kutoka Sergio Aguero na Cesc Fabregas jinsi England ilivyokuwa nzuri. Kuna mvuto wa changamoto mpya. Sasa Messi anakomaa na pia hufuatilia Ligi Kuu England. Sasa anajifunza Kiingereza akijitayarisha na Uhamisho.”
Balague amesisitiza mara kadhaa Klabu kubwa za Ulaya zimejaribu kumnunua Messi huko nyuma zikiwemo Mahasimu wa Barca, Real Madrid, na hata Arsenal.


Mchambuzi huyo amefafanua: “Wakati ule dili za kuhama Gerard Pique na Cesc Fabregas zilipokubaliwa [Pique kwenda Man United na Fabregas kwenda Arsenal] Watatu hao walikuwa Timu moja na Messi pia alifuatwa kuhamia Timu ya Wenger..Arsenal!”
Maisha yake yote ya Soka Messi amekuwa na Barcelona na kutwaa Mataji makubwa 25 pamoja na Tuzo ya Mchezaji Bora Duniani, Ballon d’Or, mara 4 ingawa katika Miaka Miwili iliyopita Ronaldo amempiku na kuitwaa.
Hivi sasa Messi yupo nje ya Uwanja akijiuguza Goti aliloumia Mwezi Septemba lakini anatarajiwa kurudi kilingeni hapo Novemba 21 kwenye El Clasico dhidi ya Real Madrid.

0 maoni:

Post a Comment

waliotembelea blog