Wednesday, August 26, 2015

.
Mwaka huu ni headlines za Uchaguzi 2015 tumeona baadhi ya wasanii wameonesha kutoa support kwenye kipindi hiki kwa wagombea Urais wawili ambao ni John Pombe Magufuli atakaegombea CCM na Edward Lowassa kupitia CHADEMA.
Miongoni mwa wasanii waliojitokeza na kutangaza rasmi kumsupport mgombea Urais kupitia CCM, Dkt.John Pombe Magufuli, kuna Wema Sepetu, Batuli, Snura, Linex, Steve Nyerere, Diamond Platnumz, Shetta, Barnaba,Bushoke, Kysher, Wastara na wengineo huku mwigizaji Aunty Ezekiel na Jackline Wolper wanamsupport Edward Lowassa na sasa ni zamu ya Nay wa Mitego.
Nay wa Mitego anamsupport Edward Lowassa kayaandika haya….>>>>
Huwezi zuia Mvua ikiamua kunyesha inanyesha tu! Tuna Imani na Lowassa. Ccm wote bado wana Imani na Lowassa hata Kura za Urais ni kwa Lowassa.Nilikua sipost chochote coz Nilikua nataka nisikie CCM labda wana jipya juu ya sera yao mwaka huu coz upinzani umekua mkali, wangenishawishi kidogo. Dooh ndo wameongeza uozo mara dufu.Watanzania wameamka si kwa uongo ule wa jana Milioni Hamsini kila Kijiji. Tanzania ina vijiji vingapi? Piga Hesabu ya haraka kadilia, si chini ya bilioni 600 na zaidi.Watanzania sio mazoba kiasi hicho tumeshtuaa…Hamjajipanga mwaka huu mmetukosa..#Mabadiliko2015

0 maoni:

Post a Comment

waliotembelea blog