Thursday, August 27, 2015

HAPA ALIAMUA KUJIFUA NA TIMU YA RUGBY ILI KUJIWEKA FITI ZAIDI.

Mtanzania Emily Mgeta sasa anajiandaa kuendelea kupasua anga katika soka la Ujerumani akiwa na kikosi chake cha Neckarsulmer.


Neckarsulmer inashiriki daraja la tano na Mgeta anaonekana taratibu kujihakikishia namba katika kikosi cha kwanza na wikiendi hii wanatarajia kucheza dhidi ya Schwäbisch Hall.

“Kweli tutacheza na Schwabisch Hall, mechi itakuwa ngumu kwa kuwa jamaa ni wazuri lakini tumepania kuendelea kufanya vema.

“Mazingira ya kazi hapa ni mazuri lakini yanataka umakini na kujituma sana kaka. Naendelea kujitahidi  nifanye vizuri zaidi,” alisema.
Mgeta aliwahi kuichezea Simba pia Polisi Moro kabla ya kuondoka Tanzania na kujiunga na Neckarsulmer 
.

Mgeta amesema anaamini kufanya vema kutamsaidia kusonga mbele kimataifa, hivyo hatachoka.

0 maoni:

Post a Comment

waliotembelea blog