Friday, July 17, 2015



Klabu ya Bayern Munich imesafiri kwa muda wa masaa tisa kutoka Ujerumani hadi  China kwa ajili ya kuweka kambi ya maandalizi ya msimu mpya wa Bundesliga, huo huwa ni utaratibu wa vilabu vingi duniani.

Kizuri zaidi kuhusu safari yao ni mapokezi walioyapata Beijing mtu wangu zilitumika dakika  30 tu kujaza  umati wa watu wasiopungua 1000 kuwapokea huku wakiombwa kusainiwa vitabu vyao vya kumbukumbu (autographs).

Watu ni wengi wanaohudhuria mazoezi yao, uwanja ukafurika kama kuna mechi. Mashabiki wamekuwa wakiomba kupiga picha na wachezaji, lakini pia wachezaji hawakuwa nyuma kuchukua kumbukumbu zao kwa kupiga picha kwa kutumia simu zao.
Wachezaji kama Philipp LahmManuel Neur na wengine wamekiri kitu kama hicho hutokea mara chache tu.
 

 

 

 

 


Hapa ninayo video pia, unaweza ukacheki love ambayo Bayern Munich waliipata wakiwa Beijing.

0 maoni:

Post a Comment

waliotembelea blog