Friday, July 17, 2015


Arsene Wenger amesema Arsenal wanalenga kuwa Mabingwa wa Ligi Kuu England Msimu huu unaoanza Agosti 8.
Msimu uliopita Arsenal walimaliza Nafasi ya 3 kwenye Ligi ambayo hawajawahi kutwaa Ubingwa tangu 2003/04 na tangu wakati huo walitoka kapa kila Msimu na kuonja Makombe Mwaka Jana kwa kutwaa FA CUP na kulitetea tena Mwaka huu.
Hadi sasa Arsenal imemsaini Mchezaji mmoja tu, Kipa Mkongwe kutoka Chelsea, Petr Cech, lakini Wenger ana imani kubwa na Kikosi chake.

Amenena: "Ubingwa ni lengo letu na tunaamini tuna nafasi ya kuleta changamoto. Hatuko mbali."
Wenger, alietua Arsenal Mwaka 1996, ameweza kuipa Ubingwa wa Ligi Kuu England mara 3 kwenye Misimu ya 1997/98, 2001/02 na 2003/04.
Kipa mpya wa Arsenal Petr CechArsene Wenger akiwaangalia Vijana wake kwenye mazoeziMtu kati!Cazorla wakati wa mapumziko

0 maoni:

Post a Comment

waliotembelea blog