Tuesday, July 28, 2015

Hamisi Kiiza (jezi namba tano) akipongezwa na wenzake jana baada ya kufunga
MSHAMBULIAJI wa kimataifa wa Uganda, Hamisi Friday Kiiza ‘Diego’ jaja amefunga bao lake la kwanza akiichezea kwa mara ya kwanza klabu yake mpya, Simba SC katika mchezo wa kirafiki dhidi ya Kombaini ya Zanzibar.
Katika mchezo huo wa kirafiki uliofanyika Uwanja wa Amaan, Zanzibar Simba SC ikicheza kwa mara ya kwanza chini ya kocha wake mpya, Muingereza Dylan Kerr iliibuka na ushindi wa mabao 2-1.
Bao lingine la Simba SC lilifungwa na Nahodha mpya wa klabu hiyo, Mussa Hassan Mgosi.


0 maoni:

Post a Comment

waliotembelea blog